05/10/2024
Kutoka katika kumbukumbu:-
Amitabh Bachchan (mwigizaji gwiji nchini India) aliwahi kusema:
"Katika kilele cha kazi yangu, wakati fulani nilikuwa nikisafiri kwa ndege. Abiria mmoja karibu yangu alikuwa bwana mzee aliyevaa shati ya kawaida sana na suruali. Alionekana kuwa mtu wa kawaida na mwenye kipato cha kawaida sana na msomi flani hivi.
Abiria wengine labda walinitambua mimi ni nani, lakini bwana huyu alionekana kutojali uwepo wangu....Alikuwa akisoma karatasi yake, akichungulia dirishani, na chai ilipotolewa, aliinywa kimya kimya.
"Nilipojaribu kuanzisha mazungumzo naye nilitabasamu. Mzee huyo naye alitabasamu kwa heshima na kusema 'Habari?'
"Tulizungumza na nikaleta mada ya sinema na kuuliza, 'Je, unatazama filamu?'
"Mzee huyo alijibu, 'Oh, mara chache sana. Niliona moja miaka mingi iliyopita.'
"Nikamwaambia kwamba ninafanya kazi katika tasnia ya sinema.
"Mzee yule akajibu .." oh, hiyo ni nzuri. Unafanya nini?'
"Nilijibu, 'Mimi ni mwigizaji'
"Mzee huyo akaongeza, 'Ah, hiyo ni nzuri!'
"Tulipotua, nilinyoosha mkono wangu na kusema," nimefurahi kusafiri pamoja nawe. Jina langu ni Amitabh Bachchan!'
"Mzee huyo alinishika mkono na kutabasamu, "Asante... nimefurahi kukutana nawe..Mimi ni J R D Tata (Mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni iitwayo TATA)!"
"Nilijifunza siku hiyo kwamba hata ujifikirie kuwa mkubwa kiasi gani, siku zote kuna mtu mkubwa zaidi.
Kuwa mnyenyekevu, haigharimu chochote"
~ Kutoka peruzi mitandaoni.
Imetafsiriwa kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili na Karume J. Asanga